Obama: Waislamu ni wahanga wa ugaidi
Rais Barack Obama wa Marekani amekiri kwamba Waislamu ni wahanga wa ugaidi.Obama ambaye alikuwa kihutubia katika shughuli za kidini mjini Washington amesisitiza kuwa Wakristo na Waislamu wamekuwa wahanga wa ugaidi na kwamba lengo la magaidi ni kudhoofisha imani za watu na kueneza chuki na mtazamo mbaya kuhusu dini na mbari tofauti.